AINA ZA SADAKA NA UTOAJI WAKE
tunapoanza
kuangalia juu ya sadaka ni muhimu kwanza kabla hatujaangalia kuhusu sadaka tuangalie mitazamo hasi juu ya sadaka
1.
Sadaka sio msaada
Watu wengi
hudhani ya kuwa sadaka ni msaada ambao mtu anatoa katika ualme wa Mungu,au ni
msaada kwaajili ya kupeleka injili,au msaada kwaajili ya nyumba ya mchungaji au
mtumishi yeyote wa Mungu
Hapana huo
ni mtazamo ambao sio wa kimaandiko hebu tuangalie hii
Warumi 11:36
36Kwa
maana vitu vyote vyatoka Kwake,
viko
Kwake na kwa ajili Yake.
Utukufu ni Wake milele.
Amen.
1 cor 8:6
6Lakini kwetu sisi yuko Mungu mmoja, aliye Baba, ambaye vitu
vyote vyatoka Kwake na kwa ajili Yake sisi twaishi na kuna Bwana mmoja tu, Yesu
Kristo, ambaye kwa Yeye vitu vyote vimekuwepo na kwa Yeye sisi tunaishi
Katika
mistari hiyo hapo juu utaona na kugundua kuwa vitu vyote ni mali ya bwana na
hakuna kitu kinachotoka kwako au kipo kwa uwezo wako,vitu vyote vyatoka kwake
na vipo kwa uweza wake na kwaajili yake,
Kwa hiyo
basi ni kosa kufikiri ya kuwa unapotoa sadaka unakuwa unatoa msaada kwa kanisa
au ufalme wa mungu au Kwa mtumishi wa Mungu.
2.
SADAKA SIO KILE UNACHOTOA
Sadaka
halisi sio kile unachotoa bali kile Kinachokusukuma kutoa,sadaka sio ile fedha
unayoweka katiaka kapu la sadaka bali ni ule moyo wako unaokusukuma kutoa
Luka 21:3
Yesu alipoinua macho
yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya hekalu.2Akamwona pia mwanamke mmoja mjane
maskini, akiweka humo sarafu mbili za shaba. 3Yesu akasema, “Amin, amin nawaambia, huyu mjane maskini ameweka
humo sadaka kubwa zaidi kuliko wengine wote.
Watu wengi
huwa wanafanya makosa wakifikiri wingi wa sadaka anayotoa ndiyo inayomfanya
mungu kuweza kuachilia Baraka katika maisha yao,bila kukumbuka kuwa ni moyo
ambao mungu huangalia
Hebu tuangalie
huo mfano hapo juu utaona ya kuwa Yule mwanamke mjane pamoja na kuwa alitoa
sarafu moja tuu na wengine wakatoa dhahabu na pesa nyingi,alionekana kuwa
mtoaji bora wa siku hiyo. Ni kitu gani kilafanya akaonekana bora kuliko
wengine,ni ule moyo wake,Ni ile nguvu au msukumo wa utoaji na kwa sababu hiyo
pamoja na kuwa alitoa kiasi kitdogo lakini alionekana ametoa kitu kikubwa zaidi
ya wengine.
1falme 17:13
13Eliya
akamwambia, “Usiogope. Nenda nyumbani ukafanye kama ulivyosema. Lakini kwanza
unifanyizie mimi mkate mdogo kutoka vile ulivyonavyo kisha uniletee na ndipo
utayarishe cho chote kwa ajili yako na mwanao. 14Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo BWANA, Mungu wa Israeli: “Lile
gudulia la unga halitakwisha wala ile chupa ya mafuta haitakauka hadi siku ile
BWANA atakapoleta mvua juu ya nchi.’’
15Akaondoka na kufanya kama Eliya alivyomwambia. Kwa hiyo
kukawa na chakula kila siku kwa ajili ya Eliya, yule mwanamke na jamaa yake. 16Kwa kuwa lile gudulia la unga
halikwisha na ile chupa ya mafuta haikukauka, sawasawa na lile neno la BWANA
alilosema Eliya.
Sasa angalia
jambo jingine hapa,na utagundua kuwa huyu mwanamke wa serepta pamoja na
mwanamke Yule mjane katika luka 21:3 wanakitu kinachofanana kinachofanya
waonekane kuwa bora zaidi ya wengine,ni ile nguvu inayo wasukuma katika
utoaji,wanatoa sio kwa sababu wanavyovingi bali ni kwasababu ya moyo wa imani
na moyo wa kupenda.
Hivo bas kwa
kukazia nataka ufahamu kuwa sadaka sio kile unachotoa ila Kipimo cha nguvu
inayosukuma sadaka.
Hebu
tuangalie mfano wa Mwisho
Mwanzo 22:1-2 &11
Uthabiti
wa Abrahamu
KujuaBaadaye Mungu akamjaribu Abrahamu.Akamwambia,
“Abrahamu!’’ Abrahamu
akajibu,
“Mimi hapa.’’
2Kisha Mungu akamwambia, “Umchukue mwanao, mwana wako wa
pekee, Isaki umpendaye, uende katika nchi ya Moria. Mtoe huko kama sadaka ya
kuteketezwa juu ya mlima mmojwapo nitakaokuambia.’’
12Akamwambia,
“Usimdhuru kijana,
wala usimtendee jambo
lolote. Sasa ninajua kwamba unamcha Mungu, kwa sababu hukunizuilia mwanao,
mwana wako wa pekee.’’
Napenda uone
jambo katika huo mfano hapo juu ambayo nimekuonesha,na unaweza ukaona ya kuwa
Mtazamo wa Mungu juu ya Ibrahimu haukuwa juu ya sadaka bali ni kutaka kujua
uchaji wa ibrahimu na kipimo cha kujua uchaji wake kilikuwa ni kumjaribu
ibrahimu kupitia kile ambacho yeye anakipenda zaidi ya kitu kingine
Kumbuka
sababu nyuma ya sadaka haikuwa isaka bali ni uchaji yaani Kipimo cha utii na
upendo wa ibrahimu kwa Mungu.
Sio watu
wengi wanaelewa kilichofichwa ndani ya andiko hilo hapo lakini hebu
tuangalie kidogo kwa ufupi
Mungu
alimwahidi ibrahimu ya kuwa angembariki na kumpa uzao,na Mpaka kufikia mwanzo
20 Mungu alikuwa ametimiza ahadi yake kwa ibrahimu maana maandiko yanasema
Mwanzo 24
Wakati huu Abrahamu
alikuwa mzee na mwenye miaka mingi, BWANA alikuwa amembariki katika kila njia.
Biblia ya
kiswahli cha kivita inasema Mungu alikuwa amembariki ibrahimu akatika kila kitu
Mpaka wakati
huo ahadi ya Mungu ilikuwa tayari imetimia isipokuwa katika uzao,na mwazo 22
mungu akatimiza ahadi yake ya uzao kwa ibrahimu. Sasa Basi Bwana Mungu alitaka
kujua ikiwa Moyo wa ibrahimu bado alikuwa tayari kuendelea kutii na kumpenda
Mungu pamoja na kuwa Mungu alionesha kumbariki tayari.
Watu wengi
mara wanapobarikiwa hupoteza kabisa moy wa Kumpenda Mungu na Kumtafuta,unaweza
ukaona wakati mtu akiwa na mahitaji hapo ndipo anapomtafuta Mungu kwa moyo wote
na kuonesha upendo mwingi kwa Mungu,lakini mara anapofanikiwa na kupata
anachotaka,hupoteza ladha ya Mungu katika maisha yake.
Kwa hiyo
basi kutokana na sababu hiyo Mungu aliamua kumjaribu ibrahimu ili kujua kipimo
cha upendo wake.
3. SADAKA SIO TAKRIMA/RUSHWA.
Katika
huduma yangu nimeona kuna makosa makubwa sana ambayo hufanyika katika mwili wa
Kristo,unaweza ukaona watumishi wa Mungu wanashawishika kuwapa nafasi watu
Mbalimbali kwa sababu tu sadaka yao kanisani huwa ni kubwa na ya kwamba
wanaouwezo kidogo kifedha,hili ni kosa kubwa
1samwel 16:7
7Lakini BWANA akamwambia Samweli, “Usitazame sura yake wala
kimo chake, kwa kuwa nimemkataa.BWANA hatazami katika vile vitu mwanadamu
avitazamavyo. Mwanadamu hutazama katika sura ya nje, lakini BWANA hutazama
moyoni
Mungu
hatazami vile mtu alivyo kisura au kifedha katika hali yoyote bali hutazama
moyo wa Mtu,yeye haangalii kiasi cha sadaka mtu anachopeleka bali hutazama moyo
wa upendo na Uchaji
Hivo basi
sisi kama watumishi wa Mungu tusiwe wepesi kupendelea watu kwa sababu ya
Muonekano wao wa Nje(Material things). Sisemi kuwa ni vibaya ama haifai
kuchagua Mtu mwenye uwezo,hapana bali ni muhimu Mwomba Mungu kwanza kabla ya
Kuchagua
Luka 6:12
12Ikawa katika siku hizo Yesu alikwenda mlimani kuomba,
akakesha usiku kucha akimwomba Mungu.13Kulipopambazuka
akawaita wanafunzi Wake, naye akachagua kumi na wawili, ambao pia aliwaita
mitume: 14Simoni aliyemwita
Petro, Andrea nduguye, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartholomayo, 15Mathayo, Thomasi. Yakobo mwana wa
Alfayo, Simoni aliyeitwa Zelote, 16Yuda
mwana wa Yakobo na Yuda Iskariote, ambaye ndiye aliyemsaliti Yesu.
Uchaguzi
wetu juu ya nani awe msaidizi katika huduma unahitaji sana kufata hiyo kanuni
ambayo yesu alianza nayo
Chochote
kinachochaguliwa kwa mwili hufanya vitu vya mwilini na wala si vitu vya kiroho
Isaya 11:2
3naye
atafurahia kumcha BWANA.
Hatahukumu
kwa yale ayaonayo kwa
macho
yake,
wala
kuamua kwa yale ayasikiayo kwa
masikio yake,
hivo basi hata
mtoaji asitoe sadaka akitegemea kupata kitu toka kwa Mtumishi au Mchungaji bali
atoe akitegemea kupata kitu kutoka kwa Bwana.
Sasa basi
baada ya kuangalia maana mbalimbali hasi(negative) kuhusu sadaka tuangalie sasa
nini Maana ya sadaka.
SADAKA NI NINI
1. Sadaka ni Nguvu ya upendo/mtazamo
wako Kwa Mungu inayodhihirishwa kupitia vitu au Kitu
Kama
tulivyoona katika vipengere vilivyopita ya kuwa sadaka ni ile nguvu nyuma ya
sadaka,au kwa lugha nyepesi ni lile lengo linalokupelekea kutoa sadaka,mara
nyingi matokeo ya kile kinachotolewa hutokana na moyo wa mtu ulivyo.
Shida ya
sadaka ya kaini haikuwa katika kile alichokitoa bali ule Moyo wake a
ndani/lengo na mtazamo wake juu ya Mungu
Tunasoma
Mwanzo 4:4
katika
baadhi ya wazaliwa wa kwanza wa mifugo yake. BWANA akamkubali Abeli pamoja na
sadaka yake, 5lakini Mungu
hakumkubali Kaini pamoja na sadaka yake. Kwa hiyo Kaini akakasirika sana, uso
wake ukawa na huzuni.
6Kisha BWANA akamwambia Kaini, “Kwa nini umekasirika? Kwa nini
uso wako una huzuni? 7Ukifanya
lililo sawa, hutakubalika?Lakini usipofanya lililo sawa, dhambi inakuvizia
mlangoni mwako, inakutamani wewe, lakini inakupasa uishinde.
Unaweza
ukaona nguvu iliyokuwa nyuma ya sadaka ya abeli ndiyo iliyomfanya abeli aweze
kutoa kilichobora, lakini pia unaweza ukaona kaini naye kutokana na moyo wake
kutokujali,na kutokumpenda Mungu alijikuta akimkasirikia Mungu kwa Kuwa sadaka
yake haikukubaliwa.
Tunachokiona
hapa ni kuwa Mungu hakuangalia sadaka bali aliangalia Moyo wa sadaka /lengo la
sadaka au msukumo uliopo wa utoaji ulilenga kitu gani.
Sasa basi
tumesema sadaka ni nguvu ya Upendo au mtazamo ulionao juu ya Mungu.
Waebrania 10:10
10Katika mapenzi hayo sisi tumetakaswa na kufanywa watakatifu
kwa njia ya sadaka ya mwili wa Yesu Kristo alioutoa mara moja tu.
Yohana 3:16
16‘‘Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa
Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa
milele. 17Kwa maana Mungu
hakumtuma Mwanawe kuuhukumu ulimwengu, bali kwa Yeye ulimwengu upate kuokolewa
Ukiangalia
hiyo mistari hapo juu utaona kuwa imebeba maana halisi ya sadaka katika
vipengele vyake
Sababu ya
Mungu kumtoa Yesu kama sadaka ni kwa sababu aliupenda ulimwengu,ni upendo ndio
uliomsukuma mungu kumtoa yesu kuwa Sadaka.
Katika hili
tunaweza kujifunza kuwa kipimo cha upendo wako kwa Kungu ndicho kinachoamua ni
kiasi gani cha sadaka unahitaji Kutoa,au thamani ya sadaka yako inatokana na
kipimo cha upendo wako
Maandiko
yanasema Mungu alimtoa Mwanae wa Pekee,maana yake ni kuwa alitoa kile
alichonacho.
Mungu
alikuwa na Mtoto mmoja tu,hakuwa na watoto wengi,ni mmoja tu na wapekee,huyo
ndiye aliyekuwa kila kitu kwake, kwa lugha ya sasa tunaweza kusema yeye ndiye
aliyekuwa Jicho na roho ya mungu.yesu alikuwa kila kitu Kwa Mungu baba
Isaya 53:2
2Alikua
mbele yake kama mche mwororo
na kama mzizi katika
nchi kavu.
Yohana 1:14
14Neno
alifanyika mwili, akakaa miongoni mwetu, nasi takauona utukufu Wake, utukufu
kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba,
amejaa neema na kweli.
Yesu hakuwa
mmoja wa watoto wa Mungu,alikuwa mwana Pekee wa Mungu. Uzao pekee wa Mungu.
Lakini
kutokana na upendo wa Baba kwetu akaamua kumtoa yesu kristo kwajili yetu.
Ni upendo
juu ya Ulimwengu ndio ulimsukuma Mungu kumwachilia Yesu.
Yohana 15:13
13Hakuna mtu mwenye upendo mkuu kuliko huu, mtu kuutoa uhai
wake kwa ajili ya rafiki zake.
angalia tena
sababu ya yesu kuutoa uhai wake kama sadaka ilikuwa ni upendo wake kwetu na Kwa
baba Yake.
Hivo basi ni
muhimu kuliweka hili moyoni ya Kuwa sadaka sio kile unachotoa bali ni ile nguvu
ya upendo wako kwa Mungu,na kazi yake,na watumishi wake ndio inayokusukuma
kutoa
Usitoe kwa
sababu unahitaji kusaidia na ndani yako hauna msukumo wowote,utakuwa unapoteza
sadaka yako.
Kabla ya
kutoa ni muhimu kwanza kufikiria juu ya yale ambayo Mungu ameyafanya katika
maisha yako,fikiri juu ya upendo wake,rehema zake,fikiri juu ya utukufu wake
kwako,ulinzi wake,pumzi yake na vile Mungu alivyokubariki,hakafu una unadeni
kiasi gani katika kumpenda yeye kama yeye anavyokupenda,ona deni la kupenda
kazi yake kama yeye anavyopenda kazi zako,kwa njia hiyo utajikuta unazaisha
chemichemi ya upendo baina yako na Mungu.
Upendo wako
usisukumwe na kitu chochote isipokuwa upendo wa Mungu kwako.
Mungu
haitaji kitu kingine kwako ila haya
Hosea 6:6
6Kwa
maana nataka rehema, wala si dhabihu,
kumkubali
Mungu zaidi kuliko sadaka za
kuteketezwa.
Maana yake
ni kuwa Mungu hahitaji mamilioni au mia tano yako,bali ule moyo wa upendo ndio
ukusukume kutoa hicho unachotoa,kwa kuwa kile unachotoa ndicho
kitakachodhihirisha kiasi cha upendo wako kwake.
Ombi: Baba
ninaomba unipe neema ya Kukupenda wewe na kujitoa kwaajili yako na Kazi yako na
watumishi wako katika Jina la Yesu.
AINA ZA SADAKA
1.
SADAKA YA MALIMBUKO
Kutoka 13:12
12inakupasa kumtolea BWANA mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo.
Wazaliwa wote wa kwanza wa kiume wa mifugo yako ni mali ya BWANA. 13Kila mzaliwa wa kwanza wa punda
utamkomboa kwa mwana kondoo, lakini kama hukumkomboa, utamvunja shingo yake.
Kila mzaliwa wa kwanza mwanaume miongoni mwa wana wenu utamkomboa.
Sadaka ya
malimbuko ni sadaka inayohusika zaidi na wazaliwa wa kwanza,ni sadaka ya
ukombozi inayotakasa kila mzaliwa wa Kwanza,na Kumkabidhi kwa Bwana.
Limbuko
maana yake ni mzaliwa wa Kwanza,na mzaliwa huyu wa kwanza anaweza akawa wa
wanyama au,binadamu au ndege.
Na maandiko
yanasema utamtolea bwana kila mzaliwa wa Kwanza kama sadaka lengo likiwa
kutakasa ama kubariki wazaliwa wengine
1korintho 15:20
Lakini sasa Kristo
amefufuka katika wafu,limbuko lao waliolala,kwa maana kwa kuwa mauti ililetwa
na Mtu kadhalika na kiyama ya wafu
ililetwa na mtu,kwa kuwa kama katika adamu wote wamekufa,kadhalika na katika
kristo wote watahuishwa.
Sasa basi
katika mistari hiyo hapo juu kuna kitu nataka tujifunze.
Yesu Kristo
ni limbuko/au mzaliwa wa kwanza katika hao walio kufa,maana yake yeye ni
mzaliwa wa kwanza kuwa hai kati ya wale waliokwisha kufa na hivo basi kwa
sababu yeye ni mzaliwa wa kwanza katika waliokufa anao uwezo wa kuwafufua
wengine ambao wamelala mauti
Kwa tafsiri
nzuri ni kuwa Kwa sababu yesu ametolewa sadaka kama limbuko sadaka yake
inaouwezo wa kuwahuisha hata wale ambao walikuwa wamekufa.
Lengo la
Mungu kuleta sadaka ya malimbuko ni kusababisha mpenyo wa Baraka za Mungu
katika vizazi vinavyofuata,kama ni vya wanyama au vya mimea au ni watu.
Tunapo
mtazama mzaliwa wa kwanza kama lango la vizazi katika familia ni muhimu tukajua
ya kuwa ili kuruhusu Mungu kuingilia mtililiko wa vizazi vyako na kufanya kile
alichokiahidi katika isaya 54:13
13Watoto
wako wote watafundishwa na BWANA,
nayo amani ya watoto
wako itakuwa kuu
unahitaji
kumwachilia mtoto wako wa Kwanza kama sadaka ya limbuko.
Kimsingi
inatakiwa kila mzaliwa wa Kwanza anapozaliwa apelekwe madhabahuni na aachwe
pale kwa sababu huyo sio wa Kwako bali ni wa Bwana Mungu
Kutoka 34:19
19“Mzaliwa
wa kwanza wa kila tumbo ni mali yangu, pamoja na wazaliwa wa kwanza wote wa
kiume wa mifugo yako, ikiwa ni wa ng’ombe au wa kondoo au mbuzi. 20Utakomboa mzaliwa wa kwanza wa punda
kwa mwana kondoo, lakini kama humkomboi, utavunja shingo yake. Utakomboa
wazaliwa wako wa kwanza wote wa kiume.
“Mtu ye yote asije
mbele zangu mikono mitupu.
lakini kwa
sababu za kiungu,Mungu ameamuru kumkomboa maana yake ni kutoa fedha kama sadaka
badala ya Mtoto kulingana na thamani utayoona kwa Mtoto wako na kulingana na
uwezo ulio nao.
Luka 2:23
23(kama ilivyoandikwa katika Sheria ya
Bwana kwamba, “Kila mtoto wa kiume kifungua mimba atawekwa wakfu kwa Bwana”), 24pia kutoa dhabihu kulingana na yale
yaliyonenwa, katika Sheria ya Bwana: “Hua wawili au makinda mawili ya njiwa
Unaweza
ukaona ya kuwa Hata yesu Kristo alihitaji kufanya hivo kwaajili ya vizazi
vinavyofuata vya mariamu na Yosefu.
2.
SADAKA YA MBEGU
Mwanzo 1:29
29Kisha Mungu akasema, “Nimewapa kila mche utoao mbegu juu ya
uso wa dunia yote na kila mti wenye matunda yenye mbegu ndani yake. Vitakuwa
kwa ajili ya chakula chenu,
Sadaka ya
mbegu ndio sadaka inayotawala Kanuni ya kupanda na Kuvuna
Tunasoma
katika
Mwanzo 8:22
22“Kwa muda
dunia idumupo,
wakati
wa kupanda na wa kuvuna,
wakati
wa baridi na wa joto,
wakati
wa kiangazi na wa masika,
mchana na usiku kamwe
havitakoma.’’
Ni amri ya
Mungu ya Kuwa Kdili nchi Idumupo majira haya ya Kupanda na kuvuna hayata
badilika,na hivyo basi kuwa ni kanuni ya uzazi kutoka kizazi hadi kizazi
Tunapoongelea
juu ya sadaka ya Mbegu tunazungumza juu ya sadaka ambayo ina lengo la
kusababisha vitu katika maisha yako inapoachiliwa katika udongo
mzuri(madhabahu)
Sadaka hii
huleta matokeo sawa na Mbegu za kawaida na hutii kanuni ya Mavuno inayosema
“chochote Mtu apandacho ndicho atakachovuna”
Galatia 6:7
7Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi.Kwa kuwa kile apandacho mtu
ndicho atakachovuna.
Kulingana na
kanuni ya uumbaji Mungu ameumba kila kitu kuwa na mbegu ndani yake,na mbegu
hiyo inapopandwa kutoa matokeo yanayofanana na kitu kilichokizaa.
Kadhalika
unapoachilia sadaka hii tegemea ya Kuwa kile kile ulichopanda ndicho
utakachovuna.
Sasa basi
hebu tuangalie Tabia za Mbegu ili pia tuweze kuelewa matokeo tutakayopata mara
tunapopanda sadaka hii madhabahuni.
A.
Mbegu inapopandwa hufa kwanza ili
kuchipua tena
Yohana 12:24
24Amin, amin, nawaambia, mbegu ya ngano isipoanguka ardhini na
kufa, hubakia kama mbegu peke yake. Lakini ikifa huzaa mbegu nyingi.
Ili mbegu
iweze kuota ni lazima iachiliwe halafu ife,lakini isipoachiliwa basi hubakia
kama kama mbegu na isilete Matunda yoyote,natamani uelewe kuwa mbegu inahitaji
Kufa ili iweze kuishi,haiitaji kunyauka inahitaji kufa
sasa basi
kama unahitaji sadaka yako kujizalisha mara mia huna budi kuiachilia katika
madhabahu sahihi ya Mungu(udongo Mzuri) ili iweze kuinuka tena
tunapo
angalia mfano wa mpanzi tunajifunza kuwa si kila mahali unapoachilia mbegu yako
basi kuna weza kukuletea matunda,Kupitia mfano huu Tuangalia madhabahu nne
ambayo mbegu inaachiliwa na matokeo yake
4Alipokuwa akipanda, baadhi zikaanguka kando ya njia, ndege
wakaja na kuzila. 5Nyingine
zikaanguka sehemu yenye mawe, ambapo hapana udongo mwingi. Zikaota haraka kwa
sababu udongo ulikuwa hauna kina. 6Lakini
jua lilipozidi, mimea hiyo ilinyauka na kukauka kwa sababu mizizi yake haikuwa
na kina. 7Mbegu nyingine
zilianguka katikati ya miiba, miiba hiyo ikakua ikazisonga.8Mbegu nyingine zilianguka kwenye
udongo mzuri ambapo zilitoa mazao, nyingine mara mia moja, nyingine mara sitini
na nyingine mara thelathini.
1.
madhabahu iliyo karibu na njia
madhabahu
hii ni madhabahu ambayo hijakaa sawa na Mungu,hakuna udongo(Uwepo wa Mungu) ni
madhabahu ambayo mara tu unapopanda mbegu yako adui huja na kuichukua,maana
yake mbegu yako hutumiwa kwaajili ya mambo yasiyo ya Ufalme wa Mungu.
Kumbuka
madhabahu imo ndani ya Moyo wa Mtumishi wa Mungu,na sio ndani ya kanisa. Na ndo
mana unapotoa sadaka sadaka haziishii kukaa ndani ya makapu pale mbele kwenye
miambari.
Wakati wa
kwanza(agano la kale) Mungu aliruhusu madhabahu za kimwili kujengwa kwa Mawe
,kuni na mote mahali alipopachagua yeye Mwenyewe,na sadaka yako ingeweza
kutolewa hapo. Ni kwa sababu agano lile lilikuwa ni kivuli cha agano jipya
Katika
kipindi hiki Mungu hujenga madhabahu ndani ya Mtumishi kupitia Neno(mawe),Maombi(kuni)
na Moto(roho Mtakatifu).
Hivyo basi
unapotoa sadaka yako,ile sadaka inatakiwa kuliwa na Mtumishi wa Mungu na
inapoingia ndani yake iingie katika madhabahu ambayo Mungu mwenyewe ameijenga.
Sasa basi
kama madhabahu hii imejengwa njiani yaani haikujengwa na roho mtakatifu bali
imejengwa kwa tama na upako basi hata ukipanda haita ota wala haita bakia.
2.
Madhabahu iliyojengwa kwenye Mwamba
Mwamba
uliozungumzwa hapa ni mwamba kama jiwe, mahali pagumu mahali ambapo hapana
udongo wa Kina, katika eneo hili Mbegu huweza kufa lakini haiwezi kuota kwa
sababu udongo wake hauna kina
Maana yake
ni kuwa madhabahu hiyo inawezekana ikawa imejengwa na Mungu lakini kwa sababu
Haina nguvu ya mungu ya Kutosha basi mbegu hufa na hivyo haioti kabisa.
3.
Madhabahu iliyokwenye miba
Aina hii ya
madhabahu ni madhabahu ambayo kimsingi inakuwa imejengwa na Mungu mwenyewe na
ipo katika udongo mzuri, lakini kwasababu ya kusongwa songwana mambo ya Dunia
kila mbegu inayopandwa hapa huota lakini hitoi matunda.
Unapopanda
sadaka yako ya aina hii Tegemea kupata kiasi kile kile ulicho panda na si
zaidi.Mtu aliyebeba madhabahu hii ni mtu mwenye wito wa kimungu Ndani yake
lakini shida yake kubwa ni kuwa hajatulia na Mungu vizuri.
4.
Madhabahu iliyo katika Udongo Mzuri
Hii ni
madhabahu ambayo iko vizuri na Moto wake unawake,ni madhababu inayotembea na
uwepo wa Mungu, nanapopanda Mbegu yako katika Madhabu hii tegemea kuvuna mia
mara thelasini mara sitini(100x60x30=???)
B.
Mbegu huzaa kile ambacho kinafanana
na ilipotoka
Mwanzo 1:29
29Kisha Mungu akasema,
“Nimewapa kila mche utoao mbegu juu ya uso wa dunia yote na kila mti wenye
matunda yenye mbegu ndani yake. Vitakuwa kwa ajili ya chakula chenu,
Hii ni
muhimu sana Kufahamu,ya Kuwa kila Mbegu huzaa kulingana na aina yake,kwa hiyo
ninamaana ya kuwa Unapopanda upendo tegemea kuvuna Upendo
Watuweng
hutamani sana Kupendwa lakini wao wenyewe hawako tayari kujitoa kupenda.
Kumbuka kila
kitu kinachokuzunguka ni Mbegu,na kila tendo unalolifanya ni Mbegu,huzaa mara
nyingi unapopanda.
Luka 6:38
38Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa. Kipimo cha kujaa na
kushindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani
mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa.”
Unapoamua
kutoa,katika mfumo wa Mbegu jua kuwa kile kile unachotoa ndicho utakachopokea
mara dufu na kushindiliwa kabisa
Kama
ukipanda mabaya maana yake utavuna mabaya
Mithali 17:13
13Ikiwa
mtu atalipa baya kwa jema,
kamwe
ubaya hautaondoka katika nyumba
yake.
Vile Mungu
amekuumba,ameyafanya maisha yako kuwa katika mfumo wa Mbegu,na kwa hiyo
chochote unachopanda tegemea ndicho utakachovuna.
C.
Mbegu huamua kiasi cha Mavuno
Tabia
nyengine ya Mbegu ni kuwa huamua kiasi cha mavuno kutokana na kiasi
ulichokipanda.
Hauwezi
kupanda mbegu moja ya mahindi halafu utegemee kuvuna shamba zima au gunia la
mahindi hiyo haiwezekani.
D.
Mbegu Hupandwa kulingana na Msimu
Unahitaji
kujua majira ya kupanda Mbegu yako na si kila wakati unapoona unataka kupanda
ni majira.
Ninakushauri
upande mbegu yako wakati ambapo kuna uhitaji udongo inahitaji mbegu.
Lakini pia
unaposikia neno la kinabii likiachiliwa juu ya maisha yako, huo ndio wakati
mzuri sana Kupanda.
KUJIFUNZA KUTENGENEZA MAZINGIRA YA
MBEGU YAKO KUZAA KUPITIA NENO LA KINABII.
Mwanzo 27:1-8
Isaki alipokuwa mzee na macho yake yalipokuwa
yamekosa nguvu asiweze kuona tena, akamwita Esau mwanawe mkubwa akamwambia,
“Mwanangu.’’
Akajibu, “Mimi hapa.’’
2Isaki akasema, “Mimi sasa ni mzee na sijui siku ya
kifo changu. 3Sasa basi, chukua
silaha zako, podo na upinde, uende nyikani, ukawinde nyama pori kwa ajili
yangu. 4Uniandalie aina ya
chakula kitamu nikipendacho uniletee nile, ili niweze kukubariki kabla
sijafa.’’
5Basi Rebeka alikuwa
akisikiliza Isaki alipokuwa akizungumza na mwanawe Esau. Esau alipoondoka
kwenda nyikani kuwinda nyama pori na kuleta, 6Rebeka akamwambia Yakobo mwanawe, “Tazama, nimemsikia baba yako
akimwambia ndugu yako Esau, 7‘Niletee
mawindo, kisha ukaniandalie chakula kitamu nile, ili niweze kukubariki mbele za
BWANA kabla sijafa.’ 8Sasa,
mwanangu, nisikilize kwa makini na ufanye yale ninayokuambia: 9Nenda sasa katika kundi ukaniletee
wana mbuzi wawili wazuri, ili niandalie chakula kitamu kwa ajili ya baba yako,
kama vile anavyotaka. 10Kisha
umpelekee baba yako ale, ili apate kukubariki kabla hajafa.”
Kila
mtumishi wa Mungu ananeno la kinabii kwaajili ya watu wa aina Fulani na neno
hili linapoachiliwa huleta matokeo yasiyo yakawaida katika maisha yako.
Lakini
ni muhimu kujua jinsi ya kufanya neno hili likaachiliwa juu yako kwaajili ya
kuleta mabadiliko
Lakini
pia napenda ufahamu kuwa neno hili haliachiliwi mpaka umepanda mbegu au umetoa
sadaka
Katika
mistari hiyo hapo juu unaweza ukaona wakati ambapo isaka anakaribia kufa alijua
ya kuwa anahitaji kuachilia muendelezo wa Baraka juu ya watoto wake,lakini pia
alifahamu ya kuwa sio rahisi kwa neno hili kutoka likiwa na uwezo wote wa
kuleta mabadiliko mpaka pale ambapo kitu kitafanyika.
“Chazah”
hili ni neno linalo maanisha mwamko wa ndani wa nabii au mtumishi wa Mungu
unaosababisha kuachiliwa kwa Baraka yako.mwamko huu huachiliwa pale Mtumishi
anapofurahi ndani yake,ni upako maalumu ambao huachiliwa tu pale Mtumishi wa
Mungu anapofurahi kutokana na jambo ambalo umelifanya
Hebu
kwa haraka tuangalie baadhi ya mifano ya kibiblia.
1sam 9:7
7Sauli akamwambia mtumishi wake, “Kama tukienda,
tutampa nini huyo mtu? Chakula kimekwisha kwenye mifuko yetu. Hatuna zawadi ya
kumpelekea huyo mtu wa Mungu. Je tuna nini?’’
8Mtumishi akamjibu tena,
akasema, “Tazama, nina fedha robo shekelia. Hiyo nitampa huyo mtu wa Mungu ili aweze kutuambia tuende kwa
njia ipi.’’ 9(Zamani katika
Israeli, kama mtu alikwenda kuuliza neno kwa Mungu, angalisema, “Njoo na twende
kwa mwonaji,’’ kwa sababu nabii wa sasa alikuwa akiitwa mwonaji
Unaweza
ukaona jamii ya Israel walijifunza juu ya jambo hili ambalo ninakufundisha
leo,kufanya kitu kwaajili ya Mtu wa Mungu ili Neno la kinabii liweze kuachiliwa
kwaajili yako
Si
watu wengi sana huwa wanaelewa hii kanuni na nimeona wengi huona kama ni wajibu
wa mtu wa Mungu kufanya kitu kwajili yao bila wao kufanya kitu kwaajili yao,hii
ndio mana wengi wanakuwa kanisani na nimasikini na hali Mtu wa Mungu analoneno
kwaajili yao ambalo linaachiliwa kwa njia ya kupanda Mbegu.
Huwezi
ukakwepa jambo hili kama unahitaji kuingia katika ulimwengu wa mafanikio ya
kiungu,ni lazima Ufanye hivo.
Jufunze
kugusa Moyo wa mtumishi wa Mungu kwa kua ndio Madhabahu ya Mungu ilipo.
1falme 17:13
13Eliya
akamwambia, “Usiogope. Nenda nyumbani ukafanye kama ulivyosema. Lakini kwanza
unifanyizie mimi mkate mdogo kutoka vile ulivyonavyo kisha uniletee na ndipo
utayarishe cho chote kwa ajili yako na mwanao. 14Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo BWANA, Mungu wa Israeli: “Lile
gudulia la unga halitakwisha wala ile chupa ya mafuta haitakauka hadi siku ile
BWANA atakapoleta mvua juu ya nchi.’’
15Akaondoka na kufanya kama Eliya alivyomwambia. Kwa hiyo
kukawa na chakula kila siku kwa ajili ya Eliya, yule mwanamke na jamaa yake. 16Kwa kuwa lile gudulia la unga
halikwisha na ile chupa ya mafuta haikukauka, sawasawa na lile neno la BWANA
alilosema Eliya.
Angalia
mfano mwengine hapo juu,unaweza jiuliza kwa nini Eliya alisema afanyiwe yeye
mkate ? hii ni kwa sababu hakuna nabii anayeweza kuachilia Baraka ikiwa ana
njaa au nyumbani kwake kuna njaa,hivo ili kuachilia Nguvu ya baraka alihitaji
kushiba kwanza yeye na moyo wake ufurahi ndio aweze kuachilia.
Na
unaweza ukaona baada ya kufanya hivyo nini kilitokea.
Kuna
mifano mingi sana ambayo tukianza kuielezea tutamaliza siku nzima.
Kwa
kumalizia sadaka aina Mbegu ni sadaka kwaajili ya Kuongeza hema yako na Mipaka
yako .Isaya 54
3.
FUNGU LA KUMI
sadaka
ya Fungu la kumi ni kanuni ya ufalme wa Mungu,na imefungwa pia katika mfumo wa
kikanuni. Yaani hii ni sehemu ya Kumi ya Mapato yako yote unayoyapata.
Mwanzo 14:20
20Abarikiwe Mungu Aliye Juu Sana,
ambaye amewaweka adui zako mkononi
mwako.’’
Ndipo Abramu akampa
Melkizedeki sehemu ya kumi ya kila kitu.
fungu
la kumi ni sadaka ambayo haikuanza leo au jana ni sadaka ambayo imekuwepo hata
kabla ya kuwepo kwa sheria,Hii ni Kanuni inayofungua malango ya Balaka katika
ghala za Ufalme wa Mungu.
Kwa
lugha nyepesi na ya Kisasa ni Kuwa fungu la Kumi na kama kodi ya ufalme
inayokufungulia njia ya kupokea vitu kutoka katika ufalme wa Mungu kama raia wa
ufalme
Fungu
la Kumi ni kanuni ambayo Mungu ameiweka ili kusukuma maisha ya watumishi wa
Mungu ili naye Mungu aweze kukufungulia Milango ya Baraka.
Kuna
uhusiano mkubwa kati ya maisha yako na ya Mtumishi wa Mungu,na kwa kadri
mtumishi wa Mungu anapofanikiwa ndivyo na wewe unavyopata nafasi ya
kusitawi,hii ni njia ya Kibiblia
Zaburi 133
Tazama jinsi ilivyo vema na
kupendeza
wakati ndugu wanapoishi pamoja
katika umoja!
2Ni kama mafuta ya thamani yaliyomiminwa
kichwani,
yakitiririka kwenye ndevu,
yakitiririka kwenye ndevu za Aroni,
mpaka kwenye upindo wa mavazi yake.
3Ni kama vile umande wa Hermoni
unavyoanguka juu ya Mlima Sayuni.
Kwa maana huko ndiko BWANA
alikoamuru baraka yake,
naam, hata uzima milele.
Hilo
andiko unaloliona linafundisha kanuni za mtiririko wa Upako wa Kufanikiwa(mafuta),maandiko
yanasema mungu anapoachia mafuta,huachia kuanzia katika ndevu za Aron(haruni)
na hushuka mpaka kwenye ndevu na mwisho ni kwenye pindo la vazi lake
Vile
ulivyo nimatokeo ya Upako unaotoka katika maisha ya mchungaji wako/kiongozi wako
wa Kiroho,anapofanikiwa unafanikiwa
Upako
huanzia kwa mchungaji(haruni)na hushuka mpaka mwisho wa pindo la vazi
lake(kanisa),hauanzii mwisho wa upindo bali juu.
Hivo
basi ungu la Kumi ni mlengo wa kuachilia mafuta ya mafanikio kutoka kwa
mtumishi wa Mungu yatakayoshuka mpaka chini kabisa ya Mshirika wa Mwisho
kanisani.
KWA
NINI MUNGU ANATAKA TUTOE FUNGU LA KUMI KWA KANISA.
Malaki 3:10
10Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba
yangu. Nijaribuni katika hili,’’ asema BWANA Mwenye Nguvu, ‘‘nanyi mwone kama
sitawafungulia madirisha ya mbinguni na kuwamwagieni baraka nyingi mpaka mkose
nafasi ya kutosha au la. 11Nami
kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu, wala
mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake,’’ asema BWANA
Mwenye Nguvu. 12‘‘Ndipo mataifa
yote yatawaita mliobarikiwa, kwa maana nchi yenu itakuwa ya kupendeza sana,’’
asema BWANA Mwenye Nguvu.
Sababu
kuu ya kuleta zaka kamili ni ili kiwemo chakula katika nyumba ya Bwana kwaajili
ya Makuhani wanaohudumu katika nyumba ya Bwana
Makuhani
ni watumishi ambao Mungu amewatenga kwaajili ya utumishi wake.ni kama walawi
katika agano la kale,Mungu ameamuru wale madhabahuni,yaani wale sadaka
zinazotolewa madhabahuni
1korinth 9:13
13Je, hamjui kwamba, watu wafanyao kazi hekaluni hupata chakula
chao kutoka hekaluni, nao wale wahudumiao madhabahuni hushiriki kile
kitolewacho madhabahuni?14Vivyo
hivyo, Bwana ameagiza kwamba wale wanaohubiri injili wapate mahitaji yao
kutokana na injili.
Fungu la
kumi na haki yao itokayo kwa MUNGU
Unapoacha
kutoa fungu la kumi lililokamilifu maandiko yanasea unamwibia Mungu na hivo
kutembea chini ya Laana
Malaki 3:8
8‘‘Je, mwanadamu atamwibia Mungu?Hata hivyo
mnaniibia.
‘‘Lakini mnauliza, ‘Tunakuibia kwa namna gani?’
‘‘Mnaniibia zaka na dhabihu.9Mko chini ya laana, ninyi taifa lote,
kwa sababu mnaniibia mimi.
Kuna
madhara makubwa ya kuto kutoa fungu la Kumi,madhara haya ni pamoja na kutembea
chini ya Laana,na unaporuhusu laana juu yako maana yake ni kuwa hautakuwa na
maendeleo yoyote yale.
Fungu
la kumi linatakiwa kutolewa na Mtu mmoja mmoja, Kanisa,na Nchi,ili mungu aweze
kuleta ulinzi na Baraka katika maisha yetu.
Malaki 3:10
10Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba
yangu. Nijaribuni katika hili,’’ asema BWANA Mwenye Nguvu, ‘‘nanyi mwone kama
sitawafungulia madirisha ya mbinguni na kuwamwagieni baraka nyingi mpaka mkose
nafasi ya kutosha au la. 11Nami
kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu, wala
mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake,’’ asema BWANA
Mwenye Nguvu. 12‘‘Ndipo mataifa
yote yatawaita mliobarikiwa, kwa maana nchi yenu itakuwa ya kupendeza sana,’’
asema BWANA Mwenye Nguvu.
4.
SADAKA YA SHUKRANI
Kumbukumbu:8:18
Bali utamkumbuka Bwana,
Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara
agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.
sadaka ya kushukuru ni sadaka Muhimu sana kwaajili
ya muendelezo wa Agano la Baraka,Ni sadaka inayoongozwa na msukumo wa Moyo wa
Shukrani,na unyenyekevu mbele za Bwana
sadaka hii ipo kutangaza matendo ya Mungu
aliyoyafanya katika maisha ya mtu,ni kumbukumbu ya kile alichokifanya Mungu
katika maisha yako,
biblia inasema
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni