COMMENTS


Jumamosi, 4 Juni 2016

ukombozi




UKOMBOZI WA MILKI YAKO NA JINSI YA KUPANUA MIPAKA YAKO KWA NJIA YA KUOMBA.




Angalizo
Tafadhali unaposoma kitini hiki jitahidi sana kufuata na kuomba kila ombi ambalo nimeliainisha ili kupata matokeo yaliyo bora zaidi
Usipige kopy kitini hiki ni vizuri ukakinunua kutoka kwa mwandishi kwa gharama yake ili Mungu akubariki.
















UKOMBOZI WA MILKI YAKO NA JINSI YA KUPANUA MIPAKA YAKO KWA NJIA YA KUOMBA.
Isaya 54:1-3
 Imba, wewe uliye tasa, wewe usiyezaa; paza sauti yako kwa kuimba, piga kelele, wewe usiyekuwa na utungu; maana watoto wake aliyeachwa ni wengi kuliko watoto wake yeye aliyeolewa, asema BWANA. 2Panua mahali pa hema yako, na wayatandaze mapazia ya maskani yako; usiwakataze; ongeza urefu wa kamba zako; vikaze vigingi vya hema yako. 3Kwa maana utaenea upande wa kuume na upande wa kushoto; na wazao wako watawamiliki mataifa; wataifanya miji iliyokuwa ukiwa kukaliwa na watu. 
Tunajua ya kuwa Mungu ametufanya kuwa wafalme na makuhani na ametupa kusudi la kumiliki katika nchi, kumiliki kwetu na kupanuka kwetu hakutatoke tu bila kujifunza ni jinsi gani tunaweza kufanya kutokea
Unaweza ukaona ya kuwa kazi ya kupanua hema na mipaka si kazi ya Mungu bali ni kazi yako mwenyewe na usipochukua hatua kamwe huwezi kufanikiwa
Kuna mambo mengine mungu anasubiri uchukue hatua ili kusudi nay eye apige hatua katika kukusaidia na hi ndiyo sababu ninakuletea muktasari wa somo hili ili yamkini upate ufahamu na uaze kushughulika
Watu wengi wanajua sana andiko hili ufunuo 5:10
Lakini si wote wamefika katika utukufu wa Andiko hili kwa sababu hawajui ni nini kinahitajika ili kufika mahali pa juu.
Kwa kuangalia andiko hilo hapo juu la isaya 54 utaona ya kuwa si Mungu anayekupanulia mipaka bali ni wewe unaye hitajika kupanua mipaka yako,kuna nafasi kubwa bado ya kumiliki kwako na kuna nafasi kubwa kwajili ya kuzaa vitu vya Kiroho.
Mtu anakuwa tasa Kwa sababu ya kuto kuchukua hatua ya imani katika kupanua hema yake na mipaka yake ili mungu aweze kumjaza vitu
Mfano Kama Yule mwanamke wakati wa elisha asingelichukua hatua ya kwenda kuazima vyombo kwa majilani zake maana yake vile alivyonavyo vingekuwa ukomo wa ujazo wake wa kimahitaji

1falme 4
.
Vipi kama petro asingalichukua hatua ya kwenda kumfuata yesu,maana yake angeendeea kuwa mvuvi wa samaki wakati kuna mahali pa juu zaidi ya kwenye biashara ya samaki
Vile ulivyo ni matokeo ya mipaka uliyoiweka mwenyewe,unaweza kwenda mbali na hapo ulipo.


INAANZA NA WEWE KUCHUKUA HATUA
Ni vema kujua Mungu hufanya kazi na watu wa imani
Waebrania 10:38
Hivo usipochukua hatua hawezi kukusaidia,kiasi kile kile unachopanua ndicho kitakachoamua ujazo wako wa Baraka.
Mungu hutumia kipimo kinachoitwa Kadri ili kuleta Ujazo wa vitu maishani mwetu,
Efeso 3:20
20 Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu; 21naam, atukuzwe katika Kanisa na katika Kristo Yesu hata vizazi vyote vya milele na milele. Amina.
Angalia mstari niliouchora kwa mstari,hii ina maana ya kuwa unahitaji kuchukua hatua ya kuongeza nguvu ndani yako ili kumfanya Mungu atengeneze mambo makubwa katika maisha yako,haiwezekani tu ukakaa ukitegemea Mungu kufaya kitu kwajili yako kabla wewe hujaanza kwanza
Kumbuka Mungu hutumia kipimo kinaitwa Kadili
Luka 6:27-38
37  Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa; msilaumu, nanyi hamtalaumiwa; achilieni, nanyi mtaachiliwa. 38Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.
neno kwa kuwa ni sawa na neno kwa kadili,kwa hiyo ujazo wako wa Umiliki na ujazo wa mipaka yako unategemea sana ni kiasi gani umeipanua hema yako na ni kiasi gani umepanua mipaka yako
mfano kwa mfanya biashara kupata faida kubwa inategemeana na ukubwa wa Biashara yake,lakini Mtu anaye fanya biashara yake Kukua sio mtu mwengine ni wewe mwenyewe kwa kuwekeza bila kuchoka.
Mtuwa Mungu ni Muhimu sana kufahamu kuwa katika ufalme wa Mungu vitu vingi sana huanza na wewe mwenyewe. Mtu mmoja amewahi kuniuliza swali hili,”kwa nini siku hizi simuoni Mungu katika Maisha yangu nina tatizo gani” Kwa mtazamo wake alijua kwa Kuwa mimi ni Nabii basi ningeweza kumwambia kuwa unajua laana za ukoo,au mapepo n.k
Lakini akashangaa ninamfungulia andiko hili
Isaya 55:6-7
6 Mtafuteni BWANA, maadamu anapatikana,
Mwiteni, maadamu yu karibu;
7 Mtu mbaya na aache njia yake,
Na mtu asiye haki aache mawazo yake;
Na amrudie BWANA,
Naye atamrehemu;
Na arejee kwa Mungu wetu,
Naye atamsamehe kabisa.
unaona sasa inaanza na wewe kumtafuta Mungu,mtafute kwa kuwa yeye anapatikana,halafu Muite  maadamu yu karibu inaanza na wewe.

mathayo 7:7-8
7 Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa; 8kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa. 
Isaya 60:1-3
Ondoka, uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja,
Na utukufu wa BWANA umekuzukia.
Usipoomba huwezi kupata,usipotafuta huwezi kuona.usipondoka huwezi kuangaza.
Ninarudia tena Mungu hutaka wewe uanze Kwanza kisha yeye atafuata, shidani kuwa watu wengi husubiri Mungu aanze kwanza bila wao kufanya chochote
Unapoanza kwanza unaithibitisha imani yako kwa Mungu,ndio maana wengi hawafanikiwi na muda unakwenda bila kuanza kwanza.
Hata unapohitaji Baraka Mungu hutaka uanze kwanza.
Kutoka 23:25
25Nanyi mtamtumikia BWANA, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako, na maji yako; nami nitakuondolea ugonjwa kati yako. 26Hapatakuwa na mwenye kuharibu mimba, wala aliye tasa, katika nchi yako; na hesabu ya siku zako nitaitimiza. 27Nitatuma utisho wangu utangulie mbele yako, nami nitawafadhaisha watu wote utakaowafikilia, nami nitawafanya hao adui zako wote wakuonyeshe maungo yao. 28Nami nitapeleka mavu mbele yako, watakaomfukuza Mhivi, na Mkanaani, na Mhiti, watoke mbele yako

Hakuna Dawa nyingine ya kufanikiwa kiMungu isipokuwa umeanza kwa utumishi.
Sasa basi umeona kuwa kila kitu kinahitaji uanze ndipo Mungu afanye,sasa ili kufika unahitaji kupanua hema yako na unahitaji kupanua mipaka yako ili umiliki na kuwa na ujazo wa Baraka zako
Baraka hazina Kikomo.

UNAHITAJI KUWA NA ELIMU YA UKOMBOZI
Si watu wengi wanaelewa hili suala ya kuwa kila kitu kinahitaji ukombozi ili uweze kukimiliki,hii ni kwasababu Dhambi ilimpa shetani ulimwengu huu na kuwa milki yake nan do mana maandiko yanamwita mungu wa dunia hii
Luka 4:5
Akampandisha juu, akamwonyesha milki zote za ulimwengu kwa dakika moja. 6Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo. 7Basi, wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako.

Dhambi ilimpa shetani umiliki wa Dunia hii na hivyo unapookoka maeneo yako hayaokoki mpaka umeyakomboa,nchi yako haiokoki mpaka umeikomboa
Mtu mmoja aliniuliza swali hili “kwa nini watu wa Mataifa wanafanikiwa sana kuliko wana wa Mungu,jibu ni rahisi sana



Luka 4:6
6Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo. 7Basi, wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako
Shetani humpa yeyote anayemsujudia kama anavyopenda mwenyewe kwa kuwa vitu vyote ni milki yake mpaka umevikomboa

Ukombozi ni njia ya kumpokonya shetani uhalali wa Umiliki. Na shetani akijua hili amewafunga wakristo wengi sana katika umasikini kwa kuwa hawaelewi umuhimu wa maombi ya ukombozi,wanadhani ukishaokoka basi ndo umeshapata kila kitu,hapana hiyo sio njia ya kibiblia.
Hii ndio maana
efeso 6:10
Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.11Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.12Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. 

Maombi ya ukombozi ni maombi ya nguvu ni maombi ya kukomboa milki,Ardhi mipaka na kila kilicho chako,vitu vingi viko mikononi mwa adui,tunahitaji kuvikomboa.

NAMNA GANI SHETANI ALIPATA HAKI YA KIAGANO YA UMILIKI WA VITU VYETU NA MIPAKA YETU.
Kwanza kabisa nataka ufahamu kuwa vitu vyote unavyoviona havikuwekwa chini ya shetani bali chini ya Mwanadamu
Mungu alimpa mwanadamu kuwa mmiliki halali wa kila kitu katika ulimwengu huu
Mwanzo 1:26
Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. 27Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. 28Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi. 29Mungu akasema, Tazama, nimewapa kila mche utoao mbegu, ulio juu ya uso wa nchi yote pia, na kila mti, ambao matunda yake yana mbegu; vitakuwa ndivyo chakula chenu;na chakula cha kila mnyama wa nchi, na cha kila ndege wa angani, na cha kila kitu kitambaacho juu ya nchi, chenye uhai; majani yote ya miche, ndiyo chakula chenu; ikawa hivyo.Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita.

Mungu hakuumba vitu kwaajili ya Shetani bali aliumba kwaajili ya mwanadamu,ili avimiliki na kuvitawala. Kwa hiyo kuwepo mikononi mwa shetani ni makosa makubwa sana ambayo yanahitaji sana yarekebishwe.

Mwanzo 1:26
Mungu alihitaji kutengeneza Aina yake itakayo ishi katika uliwengu wa nyama na Damu,na kama Mungu alivyo mfalme wa yote ndivyo mwanadamu atawale na awe mfalme wa vyote katika ulimwengu wa Damu na Nyama.
Na hii aina yake ni mwanadamu. Sasa basi unapoona umiliki wako umekuwa ni umiliki wa Mwingine ambaye hakuwa na haki hapo kwanza,inamuhuzunisha Mungu.

DHAMBI
Kupitia Dhambi shetani alipata nafasi ya kutawala na kumiliki vitu vilivyokuwa chini ya mwanadamu
1 yohana 3:8
atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi.
Kwa hiyo Dhambi inapofanyika tu shetani anapata umiliki juu yako,juu ya ardhi yako na juu ya mipaka yako,ataingia mpaka ndani ya nyumba yako na kumiliki.
Kuna uhusiano kati yako na mazingira yako na ndio mana unapofanya dhambi wewe katika ulimwengu wa roho inahesabika kuwa na nchi(ardhi) imefanya Dhambi na kwa hiyo shetani anapata mlango wa kumiliki ardhi yako.
Ezekiel 14:12
Neno la BWANA likanijia, kusema, 13Mwanadamu, nchi itakapofanya dhambi na kuniasi, kwa kukosa, nikaunyosha mkono wangu juu yake, na kulivunja tegemeo la chakula chake, na kuipelekea njaa, na kukatilia mbali mwanadamu na mnyama;
Kwa hiyo watu wanapofanya dhambi dhambi yao inaathili nchi yao,na kumpa shetani umiliki.jambo hili humkasirisha Mungu katika namna ambayo ataadhibu kila mtu na mnyama aliyepo katika hilo eneo
Lakini pia si nchi peke yake bali pia shetani hukamata anga lililopo juu yako

2 nyakati 7:13
Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwapelekea watu wangu tauni; 14ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.

Unaona athari ya dhambi? Humpa shetani umiliki wa Ardhi hivo ili Mungu hulazimika kuifunga au kuilaani ardhi na kutokana na kuwa ardhi imekamatwa Anga nalo hukamatwa na hivo Mungu hulazimika pia kulifunga Anga
Kwahiyo utaona majira yakibadilika katika maisha yako,Mitiririko ya Kifedha itabadilika,majira ya mvua yatabadilika,na mtililiko maalumu wa mipenyo ya kimaisha itabadilika
Ona
Mwanzo 3:17
Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako; 18michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni; 19kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.

Hiyo mistari hapo juu inatupa ufahamu zaidi juu ya uhusiano uliopo kati ya mahitaji yako ya kimwili na Ardhi
Angalia baada ya adamu kufanya dhambi Mungu hashughuliki kumlani Adamu bali anailaani ardhi ambayo kwayo alitolewa.
Na matokeo ya laana hiyo yalileta madhara kwa mwanadamu hata leo.
Kwa hiyo hivo ndivyo mambo yalivyo.

2. MAAGANO
Hii ni namna nyingine shetana anapata umiliki wa mipaka na vizazi,kuna idadi kubwa ya watu ambao wamefanya maagano na shetani kupitia matambiko
Inawezekana ikawa wewe umeokoka lakini huko uliko toka wanafanya Mambo hayo na kwa hiyo unakuwa umeunganishwa katika maagano hayo na hivo mipaka yako na umiliki wako pia unakuwa chini ya Adui
Hautafanikiwa mpaka umeingia katika ukombozi wa milki na mipaka yako.
Waamuzi 2:2
nanyi msifanye agano lo lote na hawa wenyeji wa nchi hii; zipomosheni nchi madhabahu zao; lakini hamkuisikia sauti yangu; je! Mmefanya haya kwa sababu gani? 3Basi kwa ajili ya hayo mimi nilisema zaidi, Mimi sitawafukuza watoke mbele zenu; lakini watakuwa kama miiba mbavuni mwenu, na miungu yao itakuwa ni tanzi kwenu.

Wenyeji wa nchi hii ni mapepo ambayo yalitawala Dunia tangia adamu alipofanya dhambi,kwa hiyo hautakiwi kufanya maagano yoyote nao
Inapotokea ukafanya maagano nayo maandiko yanasema hao mapepo na majini yatakuwa mwiba katika maendeleo yako.
Hautaenea kokote kule.

MANENO YAKO NA MTAZAMO WAKO JUU YA UMILIKI WAKO
Huu ni mlango mwengine na shetani huutumia sana katika kuhakikisha ya kuwa hupati milki yako na hata kama umeokoka maandiko yanasema
Mithali 18:21
Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi;
Na wao waupendao watakula matunda yake.

Mithali 23:7
Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo

vile unavyojiona nafsini mwako ndivyo ulivyo na ndivyo utakavyokuwa.











JINSI YA KUKOMBOA MILKI YAKO NA MIPAKA YAKO ILI UWEZE KUIPANUA.
sasa basi baada ya kuona ni jinsi Gani Shetani amepata umiliki halali wa Mali ambazo hapo kwanza hazikuwa zake tunaweza kuangalia  sasa ni jinsi Gani ninaweza kukomboa Milki yangu,na kisha nikapanua mipaka yangu kwa njia ya Maombi
Hapa nataka ufahamu tu ya Kuwa unaweza ukawa umeokoka lakini unaishi kwenye mazingira au milki ambayo haijakombolewa na hivyo ukajikuta unashindwa kupanua wigo wako wa kufanikiwa, kumbuka Nabii yohana katika
1yohana 1:2
Mpenzi, naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako kama vile roho yako ifanikiwavyo.
anasema mpenzi naomba ufanikiwe na kuwa na afya njema kama roho yako ifanikiwavyo,maana yake ni kuwa lazima yawepo mahusiano ya ukuaji kati ya roho yako na mazingira yako ya nje,sasa kama roho yako inakuwa na mazingira yako hayakui basi hapo kunatatizo ambalo linahitaji kurekebishwa na njia ya kurekebisha ni kama ifuatavyo.

1.     INGIA KWENYE MAOMBI YA TOBA KWAAJILI YAKO NA YA ARDHI YAKO
Kuna uhusiano mkubwa baina yako na Ardhi yako na hapa ninapozungumza juu ya ardhi ninamaana ya udongo wa eneo unakotokea (Kijijini) na Eneo unalokaa
Nimewahi kukutana na kesi moja ambayo kwa namna ya kawaida haiwezekani kuitatua,kijana mmoja ambaye alikuwa akifanya biashara,alihamia kutoka kwao na kuja Dar es salaam kibiashara,na alipofika akakuta mategemeo yake yamekuwa kinyume,kila alichokuwa akifanya hakifanikiwi,nilipokutana nae nikamuuliza kama amewahi kuomba kwaajili ya makazi yake mapya,akaniambia hapana,nikajua tatizo liko wapi.

Msomaji nataka ujiulize maswali haya mawili makubwa
1.     Kwanini Adamu alipofanya Dhambi Mungu hakumwadhibu Adamu na badala yake akailaani ardhi mwanzo 3:17
Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako;18michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni;19kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.

2.     Ukisoma 2nyakati 7:14
Wakati nitakapofunga mbingu ili isiwepo mvua, au nikiamuru nzige kula mazao ya nchi au nikituma tauni miongoni mwa watu wangu, 14kama watu wangu, wanaoitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha na kuomba na kuutafuta uso wangu na kuacha njia zao mbaya, basi nitasikia toka mbinguni na kuwasamehe dhambi yao na nitaiponya nchi yao. 15Sasa macho yangu yatafumbuka na masikio yangu yatasikiliza kwa makini maombi yaombwayo mahali hapa.

 Mungu anasema ikiwa watu wake walioitwa Kwa jina lake wakitubu na kuacha dhamb zao Mungu ataponya ardhi yao? Kuna uhusiano gani hapa kati ya maisha ya Mtu na ardhi
Wakati unajiuliza swali hilo nataka uunganishe na mstari huu, popote nyayo zenu zitakapokanyaka hapo nimewapa kuwa milki yenu,kuna uhusiano gani kati ya nyayo zangu na ardhi yangu
Joshua 1:3
Vipi kama nyayo zangu zikikanyaga mahali ambapo mamelaaniwa kutokana na makosa ya wenyeji wa eneo hilo,je nitamiliki kama maandiko yanavyosema?
Mtu wa Mungu kuna muunganiko wa kiungu wa kumiliki kwako au kufanikiwa kwako kupitia nyayo zako,
Ardhi hii unayoikanyaga ndio inayobeba mafanikio yako,kwa kuwa kila unachokiona kwa macho kimetoka ardhini na aridhini kitarudi
Kwa hiyo basi ikiwa utaishi mahali ambapo hapo kwanza ardhi yake iliungamanishwa na maagano ya Kichawi au ulozi jua kabisa yakuwa kama haujapakomboa kupitia maombi ya Toba si rahis sana wewe kuweza kufanikiwa
Kwa kuwa wewe utakuwa umekoka sawa,uchawi hauta kusumbua,lakini huo uchawi utakuwa umebakia katika Ardhi,na hivyo kuzuia kufanikiwa kwako katika eneo hilo.
Utakuwa ukiomba na kuomba lakini hakuna matokeo,
lakini pia ikiwa umetoka kwenu maana yake ni kuwa nyayo zako zimebeba Baraka au laana ya ardhi ya kwenu na ukaja kuishi mahali pengine kama haukujitenganisha na maagano ya kipepo ya kwenu utasababisha hata ardhi hii mpya kuto kuzalia Matunda yanayotakiwa
Hivo basi njia ya kwanza ya kumiliki kwako na kuongezeka kimipaka ni kuingia kwenye maombi ya Toba kwaajili ya Ardhi yako huku ukiruhusu Damu ya Yesu itembee kwenye Hiyo Ardhi.





3.     MFUNGE MWENYE NGUVU
Waefeso 6:12
Kwa maana kushindana kwetu si juu ya nyama na damu, bali dhidi ya falme, mamlaka, dhidi ya wakuu wa giza na majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho

Katika kila eneo au mahali kuna mtawala wake wa eneo hili, Ufalme wa shetani umejipanga vizuri sana na kiakili sana kiasi kuwa kama usipojua kucheza nao utajikuta unazunguka tu na haupigi hatua yoyote
Wakuu wa anga ni mapepo au watu ambao wanatawala anga la eneo hilo,hii ina maana kusema kuwa wameviweka vitu vyote chini yao kama milki yao,hakuna anayeweza kufanikiwa au kuchomoza bila ruhusa yao
Sasa unapoingia kwenye eneo ni lazima Baada ya Toba ingia katika kumfunga Mkuu wa Anga anayetawala katika eneo hilo, kwa kufanya hivo utakuwa umetengeneza njia ya kufanikiwa kimwili na kimaombi.

4.     VUNJA MADHABAHU ZOTE ZA BAHALI
Ingia katika maombi ya kuvunja madhabau za Kipepo, kila mahali ambapo kuna ufalme wa kiroho jua hapo kuna madhabahu za kiroho, kama ni ufalme wa Mungu au ufalme wa giza
Madhabahu ni eneo ambalo huwa ni kiunganishi cha ulimwengu wa roho kuja mwilini au ulimwengu wa mwilini kuja rohoni,ni mahali ambapo panaunganisha Mungu na watu wa eneo au mapepo na watu wa eneo
Katika eneo kukiwa na madhabahu ya kipepo maana yake watu wanaoishi hapo wameunganishwa na kufungamanishwa katika madhabahu hizo,sasa kama wewe unataka kumiliki ni lazima uzivunje madhabahu hizo.

5.     MJENGEE MUNGU WA IBRAHIMU ISAKA NA YAKOBO MADHABAHU
Ukiisha maliza kuvunja basi mjengee mungu Madhabau, Kama ishara ya kuwaunganisha watu na Mungu wao, kumbuka ufunuo 5:10 tumefanywa kuwa wafalme na makuhani, kazi ya kuhani ni hiyo, yaani kuwaunganisha/kuwapatanisha watu na Mungu wao
Kwa hiyo basi ni Muhimu kujenga madhabahu ya Mungu mahali hapo, ninamaana ya kuwa tenga eneo au mahali au chumba ambacho kitakuwa madhabahu yako au mnara wa Mungu, mahali ambapo Mungu atatawala kuanzia hapo mpaka sehemu nyingine za mji.
6.     FANYA MAOMBI YA KUITA NA KUTIISHA MALI NA UTAJIRI
Hii ni muhimu sana,kila kitu kina masikio na kina macho,na vitu vyote hutii kwa mwenye mamlaka ya eneo,hivo basi maombi haya ni maombi ya kuita kwa sauti,ni maombi ya kutiisha kila kitu katika eneo hilo viite vije kwako iambie Ardhi ikutolee matunda,iambie ardhi ikuletee watu ,ninaamini baada ya Maombi hayo utaona upenyo usio wa Kawaida.
7.      LIPE JINA JIPYA ENEO LAKO
Mwanzo 28:18
Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo, na kumimina mafuta juu yake. 19Akaita jina la mahali pale Betheli; lakini jina la mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu. 
Tangaza katika ulimwengu wa Roho,toa jina jipya kulingana na ufunuo ulionao juu ya eneo lako. Unapo lipa jina eneo maana yake unalivika eneo uwezo flani au nguvu Fulani kulingana na vile unataka



8.     INUKA ANZA KUMILIKI NA KUTAWALA
Isaya 60:1
Ondoka, uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja,
Na utukufu wa BWANA umekuzukia


Ninaimani kuwa baada ya somo hili umetoka hatua kwenda hatua,somo hili ni Muhimu sana ili uweze kufaikiwa,lipo kwaajili ya kuweka katika matendo ili kuona matokeo
Lakini mwisho kabisa ni muhimu kufahamu kuwa ufunuo 5:10 inawahusu wale ambao wameokoka tuu,kama haujampokea Yesu kuwa Mwokozi wako basi fanya hivo leo ili uingie katika jamii ya watawala.
Wasiliana nasi tafadhali au tuma ujumbe mfupi ukiwa na jina lako na mahali unapotoka ili tuweze kukuombea,.

0763712031

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni